Showing posts with label Libya. Show all posts
Showing posts with label Libya. Show all posts

Saturday, September 16, 2023

Mji wa Derna, Libya Yaangamizwa na Mafuriko! Watu zaidi ya 20,000 wahofia kufa!

Ni Mambo ambayo tumesoma kwenye biblia...mji mzima kuangamizwa!   Wiki iliyopita huko Libya mashariki ulipita Kimbunga Daniel.  Mvua ulinyesha mwingi sana hadi bwawa mbili zilipasuka na kusababisha mji wa Derna kuteketezwa kwa maji!   Ajabu, Libya ni JANGWA! Crescent Nyekundu wa Libya wanasema watu karibu 20,000 wamehofia kufa!  Ila wataalamu wamiundo mbinu wanasema kuwa tangu Rais Ghadaffi auawawa hizo Bwawa hazikutunzwa ipasavyo ndo maana zika pasuka

KWA HABARI ZAIDI BOFYA HAPA:

Wednesday, October 31, 2012

President Obama Vs. President George Bush Jr.

Jibu ni Ubaguzi! Rais Obama kwa vile mweusi wanamchambua hadi chupi. Huyo Bush Jr  kafanya maovu mengi, watu kimya!

Saturday, September 15, 2012

Maandamano Bongo Kupinga Filamu Inayodhalilisha Waislamu


Wadau, hiyo sinema. "Innocence of Muslims'  haikutengenezwa kwa idhini ya serikali ya Marekani.  Mtu yeyote Marekani anaweza kutengeneza sinema bila idhini ya serkali. Na pia FBI wanasema kuwa mtengenezaji alitumia jina feki, Sam Bacile ambaye katengeneza sinema kadhaa za ngono (Porn).  Kwa sasa Nakoula Basselly Nakoula  yuko rumande. Mnaweza kusoma habari za kufungwa kwake HAPA.  

Nakoula Basseley Nakoula aka Sam Bacile (mwenye kitambaa cheupe usoni) akipelekwa rumande usiku wa kuamkia leo

Kutoka Blogu ya Wananchi:

WAISLAMU WAJAJUU TENA,SASA NI NCHI NZIMA

WAISLAMU nchini, wanatarajia kuandamana wiki ijayo kupinga filamu iliyotengenezwa nchini Marekani na kumdhalilishaji Mtume Muhammad. Hayo yamesemwa Dar es Salaam jana na Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda, alipokuwa akizungumza na MTANZANIA kwa simu.

Kutokana na hali hiyo, Shehe Ponda amelitaka Jeshi la Polisi nchini, kutojihusisha kwa namna yoyote na harakati za kuzuia maandamano hayo.

Sheikh ponda alisema kuwa, baada ya filamu hiyo ya Marekani kumdhalilisha Mtume Muhammad, waislamu hawawezi kukaa kimya na badala yake watalazimika kuandamana kupinga udhalilishaji huo.

“Maandamano hayo yatakuwa ni ya nchi nzima, lakini kwa sasa siwezi kusema yatafanyika siku gani kwa sababu tunafanya maandalizi ya kuyafanya wiki ijayo. Najua kwa kuyasema haya, kuna watu wengine watajitokeza kuyazuia, tunatoa wito kwao mapema waache kutuingilia katika mambo ambayo ni haki yetu na tuna uhuru wa kuyafanya. Jeshi la Polisi litambue wazi kwamba, sisi waislamu hatuna fujo, ni vema wakae pembeni kabisa waache tuandamane na kutoa tamko letu, vinginevyo ni kuanzisha machafuko. Leo nimewashangaa sana hawa polisi, wamefika mahali pa kulinda watu wanaofanya maovu, nimeshangazwa na kitendo cha kuweka ulinzi katika ofisi za makao makuu ya Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) na katika ofisi za Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA). Tena katika ulinzi huo, polisi walikuwa na silaha, nashangaa sana, yaani mtu anayefanya makosa, badala ya kumkamata anaendelea kulindwa, hii haiwezekani,” alisema Shehe Ponda.
Alisema kwamba, filamu hiyo iliyotengenezwa na Wamarekani, inachochea uhasama na chuki baina ya wafuasi wa dini mbalimbali.

Kwa mujibu wa Shehe Ponda, filamu hiyo inadaiwa kutengenezwa na raia wa Israel mwenye uraia wa Marekani na kwamba imejenga mtazamo mbaya ndani ya jamii yote duniani.

Hata hivyo taarifa zilizoripotiwa na vyombo vya habari zimemtaja mtengenezaji wa filamu hiyo ya Innocence of Muslims ni Sam Bacile, ambaye aliitayarisha kwa idhini ya Serikali ya Marekani.

Taarifa hizo zimeeleza kwamba, mtengenezaji huyo amejificha kusikojulikana, ambapo Jumuiya ya Ushirikiano wa Nchi za Kiislamu (OIC) na Vatcan, zimelaani filamu hiyo inayomvunjia heshima Mtume Muhammad.

*******************************

Kutoka NEW YORK DAILY NEWS:
 
LOS ANGELES (AP) - Authorities say federal probation officers have interviewed a Southern California filmmaker linked to an anti-Islamic movie inflaming protests across the Middle East.

A Los Angeles County Sheriff's spokesman said early Saturday that 55-year-old Nakoula Basseley Nakoula was interviewed at the department's Los Cerritos station.

 Deputy Don Walker says Nakoula was not arrested and traveled voluntarily in a squad car with deputies to the station, which is near his home.

   Walker says he doesn't have information on the interview or how long it lasted.

   TV station KC says Nakoula went to the station early Saturday morning.

  Federal probation officials couldn't be reached early Saturday. Earlier they said they were investigating the activities of Nakoula, who has been convicted of financial crimes.

Wednesday, October 26, 2011

Gaddafi Aliwatendea WaTanzania Mabaya - Vita Vya Kagera


Inaelekea waTanzania wengi wamesahau historia kati ya Libya na Tanzania. Marehemu Gaddafi alikuwa rafiki yake mpenzi nduli mshenzi Dikteta Idi Amin Dada wa Uganda!  Gaddafi alitaka Amin amwoe binti yake! Gaddafi alituma wanajeshi kutoka Libya kuwasaidia Uganda katika vita vya Kagera mwaka 1978-79.  Sisi wazee tunaukumbuka huo vita na miezi kumi na nane (miaka 18) ya shida iliyofuata!  Maoni chini yameandikwa na mwanachama la kundi - Wanabidii
Gaddafi alipotembela Uganda mwaka 1973
 ...Wanabidii!


Binafsi nachukia sana kuandika bila ya ushahidi! Na zaidi sipendi kuandika "propaganda" na taarifa za uzushi; isipokuwa napenda kuandika taarifa zilizotafitiwa kwa kuandikwa na mtafiti mwenyewe (na au mwandishi aliyeandika matokeo ya utafiti au kufanya upembuzi wa utafiti husika). Takriban wiki moja sasa (tangu Alkhamis ya tarehe 20 Oktoba, 2011) uwanja wa "Wanabidii" na majukwaa mengine ya kijamii yamekuwa yakijadili "Kuuawa kwa Kanali Muammar Gaddafi" kulikofanywa na wale wanaoitwa waasi (wa NTC) wakisaidiwa na NATO wakiongozwa na Uingereza, Marekani, Ufaranza na washirika pamoja na Waarabu (Saudia na Qatar). Gaddafi ameuawa; kwa jinsi gani, kila mmoja amesoma, ameona (kwenye picha za mnato) na au kwenye picha za video!

Ninachotaka kuandika na pengine kuanzisha "mjadala" wa kiakili ni juu ya "GADDAFI KUMSAIDIA IDI AMIN DADA KWENYE VITA VYA KAGERA [UGANDA DHIDI YA TANZANIA MWAKA 1978 HADI 1979]". Napenda niweke wazi kwamba, "historia haisomwi ili kufufa 'chuki' bali husomwa kujua yaliyopita, kuyasanifu yaliyopo na kupanga mipango kwa yajayo!". Hivi ndivyo tunavyosoma historia iwe yenye kuhuzunisha au kufurahisha! Tanzania ilipigana vita na Uganda, vita iliyoitwa VITA YA KAGERA (japokuwa ilipiganwa hata ndani ya Uganda na Idi Amini Dada kufurushwa na kuikimbia Ugnda!).

Kwa ujumla, tangu pale kifo cha Muammar Gaddafi kilipotangazwa kwa mara ya kwanza na kituo cha runinga cha Al-Jazeera na kukaririwa na vituo vingine na mashirika ya habari ya kimataifa kama BBC, CNN, Reuters, Xinhua, AFP, AP na IRNA (Press Tv) kumekuwa na mchanganyiko wa "mawazo" kwa wananchi wa Tanzania juu ya "hali" ya Gaddafi kisiasa katika mtazamo wa kifalsafa...hususan wengi wa wachangiaji kwenye mijadala hiyo wanamuona Muammar Gaddafi kama "shujaa" na "mwanamapinduzi" na "kiongozi mtukuka" na "aliyejitolea kuunganisha Afrika" na hata wengine kufikia kiasi cha kuonyesha kwamba hajawahi kutokea kama Muammar Gaddafi na hata kumpa "daraja" ya kuwa "Baba wa Afrika" na mshumaa uliyozimika! Hata hivyo wengi wamesahau kamba ni Muammar Gaddafi ndiye aliyemsaidia Idi Amin Dada kwenye Vita vya Kagera! Naomba sasa tuangalie nini alifanya Gaddafi wakati wa vita vile.

Vita vinahitaji rasilimali watu (askari na wataalamu wa kijeshi), fedha za kuendeshea vita na zana (za kivita na za mawasiliano ya kivita). Kwa mujibu wa taarifa rasmi na zinazothibitishwa na taarifa rasmi za kihistoria Muammar Gadafi alimpa Idi Amin Dada usaidizi ufuatao:

1. WANAJESHI (WAPIGANAJI) 3,000 (Elfu tatu kutoka Libya na nchi zilizokuwa na mahusiano na Libya ambazo Gaddafi likuwa anazisaida na zenye uzowefu wa mazingira ya vita [military knowhow and skills on interlocustrine terrain]);

2. ZANA KAMA VIFARU AINA YA T-54, T-55, BTR, APCs, BM-21, Katyusha MRLs;

3. MIZINGA; na

4. NDEGE ZA KIJESHI AINA YA MiG-21s na Tu-22 Bomber.

Wanajeshi wa Libya waliyotumwa Uganda walikuwa katika makundi yafuatayo: ASKARI WA KAWAIDA; WANAMGAMBO; NA ASKARI WA VITA VYA MSITUNI (WENYE UZOWEFU WA VITA VYA KIENYEKI KUTOKA JANGWA LA SAHARA [MAARUFU KAMA WATUAREG KUTOKA TCHAD, NIGER, ALJERIA NA DARFUR]). Hata hivyo, shukrani za pekee kwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (TPDF) waliyefanyakazi ya ziada ya kujitoa mhanga kupigana "kiume" na hatimaye kuyashinda majeshi ya Idi Amin Dada akisaidiwa na Muammar Gaddafi. Hata ilipofika mwezi wa Aprili, 1979 na Idi Amin Dada alipopoteza udhibiti wa nchi ya Uganda aliamua "kuikimbia" Uganda na kituo chake cha kwanza kilikuwa Libya (kwa Muamar Gaddafi) na alipewa "hifadhi" ya muda na baadaye kwenda "uhamishoni" nchini Saudi Arabia (alikoishi hadi kufa kwake akiwa Jeddah).

Kwa wasomaji na "wanabidii" na wengine wanaomtazama Muammar Gaddafi kwa kusahau "aliyoyafanya" dhidi ya kumsaidia Idi Amin Dada kuendesha vita na Tanzania nadhani wana wajibu wa kujiuliza masuala haya (hii ni pamoja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inawajibu wa kusema ukweli):

1. Wamesahau "hadithi" hii ya Vita vya Kagera? Au, vita hivi vilikuwa "propaganda" ya kisiasa?

2. Gaddafi alidhamiria nini kumsaidia Idi Amin Dada aliyeapa kuisambaratisha nchi (Tanzania) na kwa kuanzia aliteka Kagera na kuifanya sehemu ya Uganda?

3. Kama Idi Amin Dada wa Uganda alitangazwa "dikteta", "bundi", "joka", "fisi mla watu", na masimulizi mengine ya kutisha (hata ya kula nyama za watu); mtu aliyekuwa akimsaidia mtu wa aina hiyo (kama Gaddafi) anaitwaje?

4. Je, historia ya Vita vya Kagera iliandikwa kwa wino "gani" hadi leo imesahaulika?

5. Au, wote wanaodhani kwamba Muammar Gaddafi ni "shujaa" wa Afrika wamezaliwa miaka ya 1980? Na kwa jinsi hiyo hawajui kilichotokea kati ya miaka ya 1978 na 1979?

Mwisho, siandiki haya katika kuwakumbusha "majonzi" wananchi wa Kagera waliyeuawa kikatili na Idi Amin Dada; siwakumbushi machungu ya kutiwa vilema vya maisha; siwakumbushi madhila ya "kubakwa" wanawake kulikofanywa na askari wa Idi Amin Dada; na wala siwakumbushi jinsi mali zao (mashamba na nyumba) zilizvyoharibiwa na "ushenzi" wa Idi Amin Dada! Nataka niwakumbushe kwamba, "hatuwezi kurudisha nyuma historia; lakini ni wajibu kuisoma ili vizazi vijavyo vipate kumbukizi yenye kujenga mujtamaa wao." Gaddafi alikuwa "rafiki" na wakati huohuo alikuwa "adui" kwa vile alikuwa na "sura mbili ndani ya moja".

Na kwa serikali (iliyoonekana kumuunga mkono); hii ni dhana (binafsi) inawezekana Muammar Gaddafi alilipa sehemu ya "maumivu" ya vita alivyomsaidia rafiki yake mpenzi Idi Amin Dada...kama ndivyo, basi ni vema watuambie! Hatuwezi kusomeshwa historia ya "uongo" juu ya Muammar Gaddafi kumbe "mtu" huyu (yaani Gaddafi) alikuwa "mtu mwema" na kiongozi "mzuri" kuliko hata Mzee Mandela na Mwalimu Nyerere...naomba tuwe "wakweli" na kwa kusisitiza: UKWELI UTATUWEKA HURU; KAMA GADDAFI ALIKUWA RAFIKI WA AFRIKA KWA NINI ALIMSAIDIA IDI AMIN DADA KUTUPIGA? TAFAKARI SEMA UKWELI JAPOKUWA UKWELI WENYEWE NI DHIDI YA NAFSI YAKO!

Bakari M Mohamed, BBA[PLM], CPSP[T], MSc (PSCM)

Sunday, October 23, 2011

Matapeli Wameanza eti WaLibya Sasa!

Hao matapeli hawana haya hata kidogo!

**************************************************

My Dear Sir/ Madam,

I am writing this mail with tears and sorrow to seek for your assistance regards to my situation since the death of my parents, I know this letter might come to you as a surprise because we have not met each other or see face to face before. My name is Kadia Abdel Fattah Younes; from Benghazi –Libya, 23 yrs old female, Religion Muslim.

 My father of blessed memory by name late General Abdel Fattah Younes who was shot death by Islamist-linked militia within the anti-Gaddafi forces on 28th July, 2011 and after two days later my mother with my two brothers was killed one early morning by the rebels as result of civil war that going on in my country Libya.

I am now writing to seek for your assistance from Ouagadougou, Burkina-Faso where I managed to escaped nearby country through the help of United Nation after the death of my parents, and now seeking asylum in Refugee Camp here in Ouagadougou, Burkina-Faso, you can find more of my story through the BBC/ http://www.bbc.co.uk/news/world-africa-14336122

 Meanwhile, the main reason why I am seeking for your assistance is because of some money my late father was deposited in one of the banks here in Burkina Faso in my name as his next of kin which amount is (Six Million Eight Hundred Thousand Dollars ($6.8M). However, I have being advised by the bank manager to look for a foreign partner who will stand as my trustee to claim the fund due to my refugee status. It is my intention to compensate you with 30% of the total money for your services and the balance shall be my capital investment in your country through your help.

 Please get back to me if you are interesting by assisting me claiming the fund, so that I will give you all the details /contact of the bank where the fund are deposited.  Honestly i want the fund to be transferred into your account before I come over to your country to continue my education, honestly I am really suffering since I arrived in this country, it is too painful, but i hope with your help I will have the fund transferred into your account to enable me to come over to your country and have a better life to live in your country.

 As soon as i receive your interest in assisting me, i will put things into action immediately. In the light of the above, i shall appreciate an urgent message indicating your ability and willingness to handle this transaction sincerely.

Yours Faithfully,
Ms. Kadia Abdel Fattah.

Friday, April 01, 2011

Utapeli - Ajidai Mtoto wa Gaddhafi

Dear sir/Madam,

My names are Saif Al Islam Ghadaffi, the son of the present president of Libya. I am contacting for an urgent assistance. As you can read and see in the media, my family is presently undergoing tough time in the hand of the masses due to his long stay in power as the president of Libya for over 40 years now. Although there is no way you can satisfy human being, my father has done so many things to better the life of our people unfortunately they never appreciated his effort instead to resulted in calling my family bad names. I have already called the international community, European Union to come down and investigate things instead of taking side without proper investigation as I know that we will be vindicated.

Pls read more: http://www.thefirstpost.co.uk/75772,people,news,lse-investigates-saif-al-islam-gaddafi-over-phd-plagiarism-claims
The International community has reached a resolution for immediate seizure of our assets both in US and the UK.
I want to request your humble assistance to receive a total sum of $65.5 million US dollars which we have succeeded in moving in cash to one of our Africa coast.
You will receive this fund directly and keep in a safe keep while I shall come down to meet you for necessary investment as may be suggested by you. You should kindly let me know your percentage as we will be ready to share whatever percentage for your assistance.

Do note that this transaction is legal and risk free.
I shall await your urgent response.
Read more on this: http://webcache.googleusercontent.com/search?hl=en&q=cache:u7eI895cFAIJ:http://www.haaretz.com/news/international/clinton-gadhafi-must-go-now-without-further-violence-or-delay-1.346257+current+problem+facing+by+gaddafi+of+libya&ct=clnk

Saif Al Islam Ghadaffi