Showing posts with label Polisi. Show all posts
Showing posts with label Polisi. Show all posts

Saturday, October 11, 2014

Vituko Vya Askari wa Trafiki

Kutoka Facebook:

Hapo zamani za kale, Askari polisi walikuwa na nidhamu wakiwa wamevaa uniform! DUH!




HUYU NDIYE AFANDE VERONICA MDEME NAMBA ZA KAZI ILIKUWA WP 8898...AMBAYE AMEFUKUZWA KAZI BAADA YA KUNYONYANA NDIMI NA AFANDE MWENZAKE WAKIWA KATIKA SARE ZA KAZI  - 




***************************

Kutoka Gazeti la MTanzania

 RENATHA KIPAKA, BUKOBA

JESHI la Polisi mkoani Kagera limewafukuza kazi askari wake watatu kwa kulifedhehesha jeshi hilo kutokana na kitendo cha kupiga picha inayowaonyesha wawili kati yao wakinyonyana ndimi wakiwa kazini.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Henry Mwaibambe, alisema kitendo kilichofanywa na askari hao kimeshusha hadhi ya jeshi.
Aliwataja askari hao waliofukuzwa ni F.7788 PC Mpaji Mwasumbi, G 2122 PC Fadhili Linga na WP.8898 Veronica Mdeme ambao wote ni wa Kikosi cha Usalama Barabarani Wilaya ya Misenyi.
Alisema PC Mpaji na WP Veronica walipiga picha inayokwenda kinyume na maadili ya Jeshi la Polisi wakiwa kazini, huku PC Fadhili akiingia matatani kwa kuwapiga picha hiyo chafu askari wenzake na kuisambaza kwenye mitandao ya kijamii.
Kamanda Mwaibambe alisema picha hiyo ilianza kuonekana katika mitandao mbalimbali ya kijamii mapema wiki hii.
Alisema askari PC Fadhili alipiga picha hiyo mwaka 2012 kwa kutumia simu yake ya kiganjani na kuitunza, lakini wiki hii aliamua kuisambaza kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kitendo ambacho ni kinyume na kazi yake.
“Napenda kuthibitisha kuwa picha hii iliyoonekana kwenye mitandao ya kijamii ni picha halisi ambayo haijachakachuliwa kabisa.
“Maadili ya kijeshi yapo kisheria na askari wetu wanafundishwa namna ya kuishi katika maisha ya utumishi wa jeshi na si vinginevyo.
“Jeshi halikubaliani na vitendo hivi, ikitokea askari kwenda kinyume lazima achukuliwe hatua kali,” alisema Kamanda Mwaibambe.
Taarifa zaidi kutoka mkoani Kagera, zinaeleza baada ya kusambazwa kwa picha hiyo na kuonekana katika mitandao ya kijamii, WP Veronica alianguka ghafla na kupoteza fahamu kwa mshtuko wa tukio hilo.
Kutokana na hali hiyo, majirani waliokuwa karibu na nyumbani kwake walilazimika kumpatia msaada na kumkimbiza hospitali kwa matibabu, ambako aliruhusiwa juzi jioni kabla ya kutiwa mbaroni.
DAR ES SALAAM
Wakati hayo yakiendelea, Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limewahamisha askari wake, WP 5863 Quine na WP 3548 Koplo Maeda kutoka Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Ilala kwa kukiuka maadili ya kazi.
Taarifa ya ndani ya Oktoba 2, mwaka huu ya Kikosi cha Usalama Barabarani Makao Makuu Dar es Salaam iliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii, imesema askari hao walisimamisha gari dogo na baada ya dereva kujitetea, waliendelea kutafuta makosa hali iliyosababisha abiria aliyekuwa mgonjwa kufariki.
Kutokana na tukio hilo, makamanda wa polisi wa wilaya zote za Mkoa wa Kipolisi wa Dar es Salaam wametakiwa kuwakumbusha askari wao kuepuka kutolazimisha kutafuta makosa ambayo hayana madhara.
“Makosa ambayo hayana madhara katika kusababisha ajali mfano ni vifaa vya kuzimia moto, rangi, kadi kutoandika anuani, motor vehicle, leseni chini ya siku 30 na kadhalika,” lilisomeka agizo hilo kwa makamanda hao wa polisi.
 

Saturday, July 12, 2014

Kuna nini Mbeya? Watu 135 Wameuawa!

Kamanda wa Polisi Mbeya Ahmed Msangi
KWA HISANI YA LUKWANGULE BLOG:

WATU 135 wameuawa katika matukio tofauti yaliyotokea mkoani Mbeya katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Julai mwaka huu.
 
Kiasi hicho cha matukio ya mauaji ni sawa na pungufu ya matukio 21 sawa na asilimia 14 ikilinganisha na yale 156 yaliyotokea katika kipindi kama hicho mwaka jana.
 
Akitoa taarifa ya utendaji wa jeshi la polisi mkoani Mbeya, Kamanda wa polisi mkoani hapa Ahmed Msangi alisema katika takwimu hizo mauaji yaliyotokana na wananchi kujichukulia sheria mikononi yalikuwa 33.
 
Alisema mauaji yaliyosababishwa na imani za kishirikina yalikuwa 23 sawa na matukio ya mauaji yaliyotokana na sababu nyingine huku matukio ya mauaji yaliyosababishwa na wivu au ugoni yalikuwa 20.
 
Matukio ya mauaji yaliyotokana na ugomvi wa majumbani yalikuwa 16, matukio ya ugomvi vilabuni 11 na matukio ya kulipiza kisasi yalikuwa tisa.
Alisema katika kipindi hicho wahamiaji haramu 159 walikamatwa kati yao 152 walikuwa raia wa Ethiopia, 23 raia wa Burundi,10 Wasomali, saba Wapakistani, wawili kutoka Malawi na mmoja akiwa ni raia wa Msumbiji.
 
“Katika kipindi hicho tumeweza kukamata bunduki 19 ambapo gobori zilikuwa 15, bastola mbili zilizotengenezwa kienyeji, Riffle moja na SMG moja. Pia zilikamatwa silaha mbili baada ya majambazi kuuawa katika jaribio la kufanya unyang’anyi. Silaha hizo ni SMG yenye namba 3514 na AK-47 namba 592058 na risasi 25 kwenye magazini,” alisema Kamanda Msangi.
 
Aliongeza kuwa katika kipindi hicho kiasi cha lita 479 za gongo pamoja na mitambo 16 ya kutengenezea pombe hiyo vilikamatwa.
 
Kilo 296 na gramu 678 na miche 314 ya bangi zilikamatwa sambamba na mashamba matatu ya bangi yenye ukubwa wa jumla ya ekari moja na robo.

Sunday, August 11, 2013

Tamko la Jeshi la Polisi Kuhusu Sakata la Sheikh Ponda

TAMKO LA JESHI LA POLISI TANZANIA KUHUSU 
SAKATA LA SHEKHE PONDA
1. MNAMO TAREHE 10, AGOSTI ,2013 MAJIRA YA SAA 8 MCHANA, MAENEO YA SHULE YA MSINGI KIWANJA CHA NDEGE MANISPAA YA MOROGORO, KULIFANYIKA KONGAMANO LA BARAZA LA EID LILILOANDALIWA NA UMOJA WA WAHADHILI MKOANI MOROGORO. DAKIKA KUMI KABLA YA KONGAMANO HILO KUMALIZIKA ALIFIKA SHEKHE PONDA ISSA PONDA AMBAYE ALIZUNGUMZA KWA MUDA MFUPI.

2. KONGAMANO HILO LILIFUNGWA MAJIRA YA SAA 12:05 JIONI AMBAPO WATU WALIANZA KUTAWANYIKA, BAADHI YAO WAKIWA WAMEZINGIRA GARI DOGO ALILOKUWA AMEPANDA SHEKHE PONDA. BAADA YA KUTOKA KATIKA ENEO HILO, ASKARI WA JESHI LA POLISI WALIZUIA GARI HILO KWA MBELE KWA NIA YA KUTAKA KUMKAMATA SHEKHE PONDA AMBAYE MPAKA SASA ANATUHUMIWA KWA KOSA LA KUTOA MANENO YA UCHOCHEZI SEHEMU MBALIMBALI HAPA NCHINI YENYE MLENGO WA KUSABABISHA UVUNJIVU WA AMANI.

3. BAAADA YA ASKARI KUTAKA KUMKAMATA, WAFUASI WAKE WALIZUIA UKAMATAJI HUO KWA KUWARUSHIA MAWE ASKARI. KUFUATIA PURUKUSHANI HIYO, ASKARI WALIPIGA RISASI HEWANI KAMA ONYO LA KUWATAWANYA.

4. KATIKA VURUGU HIZO, WAFUASI HAO WALIFANIKIWA KUMTOROSHA MTUHUMIWA. HIVI SASA IMETHIBITIKA KUWA SHEKHE PONDA YUKO KATIKA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI AKITIBIWA JERAHA KATIKA BEGA LA MKONO WA KULIA LINALODAIWA ALILIPATA KATIKA PURUKUSHANI HIZO.

5. KUFUATIA TUKIO HILO, TIMU INAYOSHIRIKISHA WAJUMBE KUTOKA JUKWAA LA HAKI JINAI IKIONGOZWA NA KAMISHINA WA JESHI LA POLISI CP ISSAYA MNGULU IMEANZA KUFANYA UCHUNGUZI WA TUKIO HILO.

6. AIDHA, JESHI LA POLISI LINATOA WITO KWA WANANCHI KUWA WATULIVU WAKATI SUALA HILI LINASHUGHULIKIWA KISHE
Imetolewa na:-
Advera Senso- SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.

Saturday, August 10, 2013

Sheikh Ponda ApIgwa Risasi Na Polisi Morogoro!

Sheikh Ponda Issa Ponda


Mda kama dakika 20 zilizopita  mjini Morogoro shehe Ponda amepigwa risasi na polisi .
Inasemekana pengine umauti umemkuta .

Dhahama hiyo imempata baada ya kushuka kwenye tax ambako kulikuwa leo
akiendesha mhadhala baada ya mhadhala huo kukawa kama kuna maandamano
kueleke barabarani, gafla polisi walitokea na kuanzanza kutawanya wakati huo yeye
alikuwa hayupo .

Ndipo mda mdogo akawasili akashuka na ndipo akapigwa risasi za kutosha.

 UPDATE:

Haijulikani hali yake. RPC, Faustine Shilogile, anasema hali ni shwari ila Ponda hajui hali yake Maana polisi walizuia gari la Ponda wamkamate, lakini wananchi wakaanza kushambulia polisi ndipo wakarusha risasi hewani kutawanya watu, lakini wananchi wakamtorosha. Anasema taarifa ni nyingi za uongo, hakuna watu polisi wala hospitali waliozingira na anaomba anayejua alipo atoe taarifa.


Chanzo: http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/502527-sheikh-ponda-ajeruhiwa-vibaya-baada-ya-kupigwa-risasi-kwenye-mhadhara.html#post7045479

*************************************************

 From All Africa.Com

Tanzania: DPP Directs Arrest of Sheikh Ponda for Disobeying Order


Sheikh Ponda was in May, convicted of forcible entry into a plot by the Kisutu Resident Magistrate's Court in Dar es Salaam. He was given a oneyear suspended jail term and directed to refrain from taking part in incitement activities likely to lead to breach of the peace in the country.
Dr Feleshi noted that recent reports have it that the cleric is engaged in organising religious gatherings in Zanzibar, which threatened peace in the Isles. "Such a behaviour is intolerable," the DPP said in an interview with the 'Daily News' on Wednesday.
He added: "We hope the police will exercise their powers wisely to arrest Sheikh Ponda and take him to court for penal actions." Dr Feleshi said what Sheikh Ponda was currently doing was contrary to his sentence. "He was convicted of a similar offence, but was still conducting acts that threaten the public order and concord.
This is not acceptable. We cannot let one disobey court orders and go on unpunished," he said. Counsel for Sheikh Ponda Juma Nassoro was not reached for comment on the matter.
Reports from Zanzibar have it that police are tracing Sheikh Ponda's whereabouts. He is alleged to have called on the citizens to initiate strikes against the government. Zanzibar Commissioner of Police, Mussa Ali Mussa was reported to have said that Ponda's statements breached police directives to religious leaders to avoid giving messages which threaten the country's peace.
The police in the Isles arrested five persons who reportedly gave shelter to the controversial Muslim Sheikh. They were interrogated for hosting Ponda.
Sheikh Ponda, according to the police, had requested the believers to be ready to fight for their rights and stressed that they should soldier on.
Adjourning the Zanzibar House of Reps budget session for 2013/2014, the Second Vice-President, Amb. Seif Ali Iddi announced a ban for Sheikh Ponda to set his foot in the Isles for the purpose of inciting the people. Amb. Iddi warned that the government should not be blamed for serious measures that would take against leaders of such calibre

Saturday, September 15, 2012

Maandamano Bongo Kupinga Filamu Inayodhalilisha Waislamu


Wadau, hiyo sinema. "Innocence of Muslims'  haikutengenezwa kwa idhini ya serikali ya Marekani.  Mtu yeyote Marekani anaweza kutengeneza sinema bila idhini ya serkali. Na pia FBI wanasema kuwa mtengenezaji alitumia jina feki, Sam Bacile ambaye katengeneza sinema kadhaa za ngono (Porn).  Kwa sasa Nakoula Basselly Nakoula  yuko rumande. Mnaweza kusoma habari za kufungwa kwake HAPA.  

Nakoula Basseley Nakoula aka Sam Bacile (mwenye kitambaa cheupe usoni) akipelekwa rumande usiku wa kuamkia leo

Kutoka Blogu ya Wananchi:

WAISLAMU WAJAJUU TENA,SASA NI NCHI NZIMA

WAISLAMU nchini, wanatarajia kuandamana wiki ijayo kupinga filamu iliyotengenezwa nchini Marekani na kumdhalilishaji Mtume Muhammad. Hayo yamesemwa Dar es Salaam jana na Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda, alipokuwa akizungumza na MTANZANIA kwa simu.

Kutokana na hali hiyo, Shehe Ponda amelitaka Jeshi la Polisi nchini, kutojihusisha kwa namna yoyote na harakati za kuzuia maandamano hayo.

Sheikh ponda alisema kuwa, baada ya filamu hiyo ya Marekani kumdhalilisha Mtume Muhammad, waislamu hawawezi kukaa kimya na badala yake watalazimika kuandamana kupinga udhalilishaji huo.

“Maandamano hayo yatakuwa ni ya nchi nzima, lakini kwa sasa siwezi kusema yatafanyika siku gani kwa sababu tunafanya maandalizi ya kuyafanya wiki ijayo. Najua kwa kuyasema haya, kuna watu wengine watajitokeza kuyazuia, tunatoa wito kwao mapema waache kutuingilia katika mambo ambayo ni haki yetu na tuna uhuru wa kuyafanya. Jeshi la Polisi litambue wazi kwamba, sisi waislamu hatuna fujo, ni vema wakae pembeni kabisa waache tuandamane na kutoa tamko letu, vinginevyo ni kuanzisha machafuko. Leo nimewashangaa sana hawa polisi, wamefika mahali pa kulinda watu wanaofanya maovu, nimeshangazwa na kitendo cha kuweka ulinzi katika ofisi za makao makuu ya Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) na katika ofisi za Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA). Tena katika ulinzi huo, polisi walikuwa na silaha, nashangaa sana, yaani mtu anayefanya makosa, badala ya kumkamata anaendelea kulindwa, hii haiwezekani,” alisema Shehe Ponda.
Alisema kwamba, filamu hiyo iliyotengenezwa na Wamarekani, inachochea uhasama na chuki baina ya wafuasi wa dini mbalimbali.

Kwa mujibu wa Shehe Ponda, filamu hiyo inadaiwa kutengenezwa na raia wa Israel mwenye uraia wa Marekani na kwamba imejenga mtazamo mbaya ndani ya jamii yote duniani.

Hata hivyo taarifa zilizoripotiwa na vyombo vya habari zimemtaja mtengenezaji wa filamu hiyo ya Innocence of Muslims ni Sam Bacile, ambaye aliitayarisha kwa idhini ya Serikali ya Marekani.

Taarifa hizo zimeeleza kwamba, mtengenezaji huyo amejificha kusikojulikana, ambapo Jumuiya ya Ushirikiano wa Nchi za Kiislamu (OIC) na Vatcan, zimelaani filamu hiyo inayomvunjia heshima Mtume Muhammad.

*******************************

Kutoka NEW YORK DAILY NEWS:
 
LOS ANGELES (AP) - Authorities say federal probation officers have interviewed a Southern California filmmaker linked to an anti-Islamic movie inflaming protests across the Middle East.

A Los Angeles County Sheriff's spokesman said early Saturday that 55-year-old Nakoula Basseley Nakoula was interviewed at the department's Los Cerritos station.

 Deputy Don Walker says Nakoula was not arrested and traveled voluntarily in a squad car with deputies to the station, which is near his home.

   Walker says he doesn't have information on the interview or how long it lasted.

   TV station KC says Nakoula went to the station early Saturday morning.

  Federal probation officials couldn't be reached early Saturday. Earlier they said they were investigating the activities of Nakoula, who has been convicted of financial crimes.

Tuesday, September 04, 2012

Mauaji Iringa Yamtesa IGP Mwema!

Kutola Gazeti la Mwananchi

Tanzania Inspector General of Poice Mr. Said Mwema

Mauaji Iringa Yamtesa

Tuesday, 04 September 2012
AJICHIMBIA KUTETA NA VIGOGO WA POLISI, VIONGOZI CHADEMA, DK NCHIMBI AKATISHA ZIARA AREJEA NCHINI

Waandishi Wetu

TUKIO la kuuawa kwa mwandishi wa habari wakati polisi wakipambana na wafuasi wa Chadema mkoani Iringa, limelitikisa jeshi hilo na jana Mkuu wake (IGP), Said Mwema alilazimika kujifungia na vigogo wa polisi Mkoa wa Iringa kujadili suala hilo.

Wakati IGP Mwema akifanya mkutano huo, uliodumu kwa zaidi ya saa mbili na nusu, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi amelazimika kukatisha ziara yake ya kikazi Afrika Kusini na kurejea nchini kushughulikia suala hilo.

Mwema alienda Iringa jana na kuitisha mkutano huo uliowahusisha pia viongozi wa Chadema, akiwamo Katibu Mkuu wake, Dk Willibrod Slaa katika mazingira yaliyoelezwa kuwa na ulinzi mkali.

Hii ni mara ya kwanza IGP Mwema kwenda mwenyewe kwenye mikoa kunakotokea vurugu kati na vyama vya siasa na baadaye mauaji ya raia.

Julai 15, mwaka huu vurugu za aina hiyo zilitokea mkoani Singida ambako Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM Kata ya Ndago wilayani Iramba, Yohana Mpinga aliuawa kwa kupigwa na silaha za jadi.

Pia mkoani Morogoro, Ally Zona aliuawa katika vurugu zilizoibuka baina ya polisi na wafuasi wa Chadema katika haraka za jeshi hilo kuwasambaratisha wafuasi hao kwa kile ilichoeleza kuwa maandamano yao yalipigwa marufuku.

Katika vurugu zote hizo, IGP amekuwa akituma wawakilishi au kutumia polisi kwenye mkoa husika kushughulikia matatizo hayo.

Makubaliano ya Kikao

Taarifa kutoka ndani ya kikao hicho zimeeleza kuwa polisi imekubaliana na Chadema na Umoja wa Vyama vya Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) kusitisha majadiliano yote yanayohusu kifo cha mwandishi huyo hadi mazishi yake yatakapokamilika.

Mwenyekiti wa UTPC, Kenneth Simbaya alisema baada ya mkutano huo kuwa wamekubaliana kuwa na mkutano mwingine baada ya shughuli za mazishi kukamilika.

“Tulichoomba kifanyike ni kwamba, tumzike mwenzetu halafu majadiliano mengine juu ya ilikuwaje kwa nini na nini kifanyike kwa siku za usoni yatakuja,” alisema Simbaya.

Alisema sasa wanasubiri mwili wa Mwangosi ufanyiwe uchunguzi na wataalamu kutoka Dar es Salaam kabla ya kukabidhiwa kwa ndugu kwa ajili ya maandalizi ya mazishi.

Katibu wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Iringa (IPC), Francis Godwin alisema uchunguzi wa awali wa IPC unapingana kwa asilimia zote na taarifa ya jeshi hilo kwa kuzingatia taarifa zilizotolewa na baadhi ya waandishi waliokuwapo katika tukio hilo.

“Taarifa kutoka katika vyanzo vyetu zinaonyesha kwamba Mwangosi alipigwa kwa virungu kabla ya kulipuliwa na bomu hilo ambalo kwa vyovyote vile mhusika wake mkuu anaweza kuwa jeshi hilo na ili taarifa hiyo potofu isiendelee kuugubika umma, IPC imeamua kutoa tamko linalolenga kuviarifu vyombo huru viingilie kati uchunguzi,” alisema Godwin.

Nchimbi Katisha Ziara

Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Nchimbi jana alilazimika kukatisha ziara yake ya kikazi, Afrika Kusini na kurudi nchini ambako pamoja na mambo mengine, atazungumza na waandishi wa habari leo kuhusu tukio hilo.

Nchimbi anarejea nchini wakati Naibu wake, Pereira Ame Silima akikataa kulizungumzia akisema uchunguzi umeshaanza.

Silima alisema tukio hilo linachunguzwa kwa pamoja kati ya Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba na IGP Mwema... “Mwema na Manumba wanaelekea Iringa ikiwa ni sehemu ya uchunguzi wa tukio hilo na baadaye ndipo jeshi la polisi litaweza kueleza ni kitu gani hasa kimetokea.”

Alisema kwa sasa lolote litakalozungumzwa juu ya tukio hilo litakuwa ni hisia tu na ukweli utajulikana baada ya uchunguzi huo kukamilika.

ongozi wa kampuni ya Africa Media Group ambao wanamiliki Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, umeitaka Serikali kuanzisha uchunguzi huru ili kubaini sababu na mazingira ya kuuawa kwa mwandishi huyo ambaye alijiunga na kampuni hiyo mwaka 2006.

Taarifa iliyotolewa na kampuni na kusainiwa na Mhariri Mkuu wa Channel Ten, Dina Chahali imetaka uchunguzi huru kufanyika na kuhakikisha wahusika wa tukio hilo wanachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

“Tunalaani vikali tukio hili ambalo halikubaliki kwa jinsi yoyote ile, tunataka kuanzishwa uchunguzi huru na hatimaye nguvu za kisheria zitumike,” imesema sehemu ya taarifa hiyo.

CHADEMA Yamtaka Rais Kikwete Kuwawajibisha Polisi!

Mkurugenzi wa Habari na Uenezi Chadema, John Mnyika akionesha picha ya polisi wakizingira Ofisi ya Tawi la chama hicho katika Kijiji cha Nyololo, Mufindi iliyochapishwa na gazeti la Tanzania Daima

DAR ES SALAAM, Tanzania


CHAMA cha Demokrasi na Maendelea (Chadema), kimemtaka Rais Jakaya Kikwete kuwasimamisha kazi vigogo wote wa Jeshi la Polisi, ambao wamekuwa wakitoa taarifa mbalimbali za uongo kuhusu mauaji ya mwandishi Daudi Mwangosi, ama awatake wajiuzuru nyadhifa zao, kupisha uchunguzi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa chama hicho, John Mnyika, aliwataja vigogo hao wa polisi kuwa ni Kamanda wa Operesheni wa Polisi, Paul Chagonja na RPC wa Iringa, Michael Kamuhanda

Wawili hao kwa mujibu wa Mnyika, kwa nyakati tofauti walidai kuwa marehemu alifikwa na mauti baada ya kuchoropoka kutoka kwa kundi la wafuasi wa Chadema na kukimbilia mikononi mwa Polisi na ghafla kulitokea mlipuko wa bomu la machozi uliosababisha kifo chake, jambo ambalo sio la kweli.

Mnyika alisema maneno hayo yanayotafuatiana na kuyaita kuwa ni ya uongo ukizingatia kwamba picha mbalimbali zimeonesha ikiwemo waandishi waliokuwemo eneo la tukio kutoa ushuhuda wao.

Kutokana na hali hiyo, Mkurugenzi huyo alisema ipo haja ya vigogo hao kung’oka kupisha uchunguzi, ili uweze kufanyika kwa haki na kuongeza kwamba Rais atumie madaraka yake kuhakikisha askari saba wanaoonekana katika picha 'wakimsghulikia' marehemu kukamatwa haraka na kuhojiwa ni nani alifyatua bunduki, kwa namna gani na vigogo gani walitoa amri hiyo.

Kwa mujibu wa Mnyika, Polisi imekuwa na tabia ya kukamata raia wanaokuwa eneo la tukio pindi kunapotokea mauaji kama hayo, hivyo ni wakati sasa wa Polisi wanaoonekana katika picha wakimshambulia marehemu Mwangosi nao kukamatwa.

Aidha alilitaka Jeshi la Polisi nchini lisitumie vibaya fedha za walipa kodi kwa kuchunguza nani alihusika na mauaji hayo wakati wauaji wanaonekana.

Mwandishi wa Habari Auwawa na Polisi Bongo!

The Late Daudi Mwangosi
Tanzanian Journalist Killed Reporting Police-Opposition Clash

               SEE HOW HE WA MURDERED AND HIS BODY MUTILATED HERE:
By Fumbuka Ng'wanakilala

DAR ES SALAAM
Tue Sep 4, 2012
DAR ES SALAAM (Reuters) - A leading Tanzanian editor accused police on Tuesday of beating up and killing television journalist Daudi Mwangosi, who died on Sunday during clashes between anti-riot police and supporters of the opposition CHADEMA party.

A police commissioner denied police responsibility but said he had ordered a joint military-police inquiry into the killing. Photos of the victim were uploaded onto the Internet and published by local newspapers.

Opposition leaders and activists linked the incident to a wider trend of rapidly growing violence against dissent in Tanzania and called for an independent inquiry.

Mwangosi was killed in a village in the Iringa region, about 500 km (315 miles) west of the capital Dar es Salaam, while reporting the clashes between police and CHADEMA supporters.

It was the first time in modern Tanzanian history that a journalist had been killed while doing his job, the Tanzania Editors' Forum (TEF) said.

"It was a deliberate move by the police, who clearly targeted this journalist. Eyewitnesses said the journalist was surrounded by police, beaten up and brutally killed," TEF secretary-general Neville Meena told Reuters.

Police fired a tear gas shell into Daudi's stomach at close range, Meena said. "Photos of fragments of Daudi's blown-up body hit the Internet less than one hour after the incident. We believe that the police are deliberately targeting journalists in a violent crackdown."

The police denied responsibility and said they had moved in to disperse an illegal gathering of opposition supporters.

"Police deny any deliberate involvement in the death of the journalist," police commissioner of operations Paul Chagonja said in a statement. "A commission of inquiry comprising officials from the police and military has been formed to investigate the death of the journalist."

Journalists at the scene uploaded images onto the Internet that they said showed Mwangosi's mutilated body lying on the ground, his abdomen ripped open and intestines spilling out.

Local newspapers published photos that showed a man lying on the ground, surrounded by anti-riot police officers who were beating him. The newspapers identified the man as Mwangosi, though the face was not recognizable.

"We condemn the killing ..." the Guardian newspaper of Tanzania said in an editorial. "It is unacceptable for the government and the public to rely on police investigations, knowing only too well that they are in this case one of the parties being blamed for the death of our colleague," it added.

Mwangosi's death came a week after one person was killed and several were wounded when police fired tear gas to break up an opposition protest in Morogoro town, a stronghold of the ruling CCM party.

(Editing by Yara Bayoumy and Tim Pearce)

MNAWEZA KUONA PICHA ZA MAUJI NA MAZISHI YA MAREHEMU DAUDI KWA KUBOFYA HAPA:

Monday, August 27, 2012

Polisi Waua Morogoro Leo!

Marehemu Ally Zona,  alikuwa ni muuza magazeti. Alipigwa risasi kichwani akiwa ameshika magaztei yake!  Hiyo jieraha inaonyesha kuwa marehemu alikuwa anakimbia kutoka kwa polisi. Alipigwa kwa nyuma.


Hapo awali ilielezwa kuwa wakati Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kikisitiza kufanya maandamano leo kisha mkutano mkubwa wa hadhara, kuliibuka mvutano baina yake na Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro, kufuatia Kamanda wake, Faustine Shilogile kupiga marufuku mandamano hayo.

Kamanda Shilogile alieleza sababu za kuzuia maandamano hayo kuwa ni udogo wa barabara za Morogoro na kwamba leo ni siku ya kazi hivyo yanawezesha kusababisha usumbufu kwa wakazi wa mji huo.

Wakati Shilogile akieleza kuzuia maandamano yanayotarajiwa kuanza saa 5 asubuhi, Mkuu wa Operesheni Sangara, Benson Kigaila, alisisitiza kuwa watafanya maandamano kwa kuwa waliskubaliana na Kamanda Shilogile kabla ya kuwageuka.

Kwa mujibu wa Gazeti la Nipashe la 27 August 2012, ilielezwa kuwa Kamanda Shilogile alidai kuruhusu baiskeli na watu kutumia barabara kwa sababu ya mikutano ya Chadema itakuwa ni kuwanyima haki wananchi wengine, na hivyo wataruhusu watu wasiozidi 50 kupita kwa wakati mmoja pasipo kuwa na ishara ya kuonyesha kama wanaelekea katika maandamano.

Pichani ni kijana aliyeelezwa kupigwa risasi kichwani katika tafrani hizo na baadae kupoteza maisha Ametambulishwa kwa jina la Ally Zona, ambae alikuwa ansoma magazeti katika stendi ya Msamvu. Tukio hili lilitokea mapema leo asubuhi kuelekea saa sita mchana wakati Polisi walipokuwa wakiwatawanya wafuasi hao wa chadema. Mtoa taarifa anasema Polisi wanadaiwa kutumia risasi za moto pamoja na mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya waandamani hao.

Watu wengine waliojeruhiwa katika tafrani hiyo wameelezwa kuwa ni mwenesha baiskeli Hashim Seif ambae amejeruhiwa kwa risasi mguuni akiwa napita na baiskeli yake na kijana mwingine aliielezwa kuwa ni muuza matunda Frank Valimba ambae amejeruhiwa na risasi tumboni.


KWA HABARI NA PICHA ZAIDI TEMBELEA KIBONGO BONGO BLOG:

********************************
TAMKO KUTOKA TANZANIA JOURNALIST ALLIANCE (TAJOA)


Jumuia ya Waandishi wa Habari Tanzania (Tajoa) inalaani kwa nguvu zote mauaji ya makusudi yaliyofanywa na Jeshi la Polisi leo mjini Morogro. Inashangaza Tanzania sasa inataka kugeuka taifa la polisi wauaji. NI vyema busara, ujuzi na mbinu stahiki zikatumika badala ya kuendelea kuua raia hata wasiokuwa na hatia.

Hebu ona huyu masikini alivyouawa kwa kupigwa risasi kwenye paji lake la uso na kumsab
abishia kifo cha papo hapo. Inaelezwa alikuwa muuza magazeti aliyekuwa kibandani kwake. Sasa tusubiri taaria ya Polisi ambayo huenda ikasema alikuwa amebeba silaha.

Tanzania, tusikubali kuwa taifa la polisi wauaji.

Marafiki wa Tajoa, nini sasa kifanyike kukomesha hali hii ambayo inaonekana kuota mizizi? Toa maoni yako hapa ili nasi tuyapeleke kwa Jeshi la Polisi

— 
Wafuasi wa Chadema wakiwa na maandamao hayo mjini Morogoro


Moshi wa mabomu yaliolipuliwa kutawanya maandamano ya Chadema leo mjini Morogoro

Akina Mama wakikimbia mabomu ya machozi

Saturday, April 07, 2012

Saturday, February 18, 2012

Dk. Mwakyembe Amjibu DCI Manumba!


Dr. Harrison Mwakyembe (picha kutoka JamiiForums.com)

           Dk. Harrison G. Mwakyembe (Mb), NW-UJ
Dar es Salaam
18/02/12
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Nimelazimika leo Jumamosi, tarehe 18 Februari, 2012 kutoa taarifa hii kwa vyombo vya habari kufuatia mkutano wa DCI Robert Manumba na waandishi wa habari jana (17/02/12) kuongelea, pamoja na mambo mengine, hali yangu ya afya na kuhitimisha, kienyejienyeji tu kuwa “sikunyweshwa sumu” ila naumwa tu ugonjwa wa ngozi bila kufafanua ugonjwa huo wa ngozi umesababishwa na nini!
Napenda nisisitize mapema kabisa kuwa msimamo huo wa Jeshi la Polisi umenikera sana katika hali niliyonayo ya ugonjwa, kwanza kwa kuingilia mchakato wa matibabu yangu na uchunguzi wa kina kuhusu kiini chake unaoendelea hospitali ya Apollo nchini India ambako bado sijahitimisha matibabu yangu; pili kwa ufinyu wa uelewa unaojitokeza bayana kwenye tamko la Jeshi la Polisi unaosisitiza kuwa “sikunyweshwa sumu” wakati sumu si lazima unyweshwe ili ikudhuru, inaweza kudhuru hata kwa kugusishwa tu; na tatu kwa Jeshi la Polisi kujiingiza kwenye suala ambalo kwa takriban mwaka mzima halijawahi kuwa na dhamira ya dhati ya kulielewa au kulichunguza mbali na kulifanyia mzaha kupitia magazetini.
Itakumbukwa kuwa tarehe 9 Februari, 2011 nilimwandikia barua IGP Said Mwema kumtaarifu kuhusu njama za kuondoa maisha yangu na ya viongozi wengine. Kwa kutambua kuwa Jeshi la Polisi la Tanzania daima husisitiza kuletewa ushahidi kwanza ndipo lifanyekazi, nilihakikisha nimeainisha katika barua  hiyo kila ushahidi nilioupata au kupewa. (Utaratibu huu wa Jeshi la Polisi kusubiri kuletewa ushahidi mezani, kama ambavyo mahakimu wanavyosubiri ushahidi mahakamani, haupo popote pale duniani (ila Tanzania tu) kwani kazi ya msingi ya Polisi si kuletewa, ni kutafuta ushahidi. Polisi wanachohitaji duniani kote ni kupata clue au tetesi tu. Hiyo inatosha kufukua ushahidi wote unaohitajika). Pamoja na kujitahidi kuanika kila aina ya ushahidi niliokuwa nao, mambo manne yalijitokeza ambayo yalionyesha wazi kuwa Polisi hawakuwa na dhamira ya dhati ya kupeleleza suala hilo:
(i)                Siku chache baada ya kumkabidhi IGP barua hiyo, nilitumiwa timu ya “wapelelezi” ofisini kwangu kuja kuchukua maelezo yangu ya ziada. Timu hiyo ilikuwa inaongozwa na ACP Mkumbo, afisa wa polisi ambaye wiki chache zilizokuwa zimepita alikuwa miongoni mwa askari waliotuhumiwa kupokea rushwa kwa lengo la kumbambikizia madawa ya kulevya mtoto wa Mwenyekiti wa IPP, Reginald Mengi, suala ambalo mpaka leo hii uongozi wa Polisi umeshindwa kulitolea maelezo ya kuridhisha. Kwa msingi huo, nilikuwa nimeletewa mtuhumiwa wa rushwa/ ujambazi kuendesha uchunguzi wa watuhumiwa wengine wa ujambazi! Nikatambua mara moja kuwa zoezi zima lilikuwa la mzaha, tena mzaha mkubwa!
(ii)              Wiki chache baada ya barua yangu kuwasilishwa kwa IGP na timu ya ACP Mkumbo “kuanza kazi”, Jeshi la Polisi likachukua hatua ya kuwapongeza na kuwazawadia askari niliowatuhumu kushirikiana na majambazi! Huhitaji kuwa profesa wa falsafa kuelewa kuwa huo ulikuwa ujumbe tosha wa kunipuuza.
(iii)            Hivi karibuni tuhuma za askari polisi kujihusisha na vitendo vya ujambazi mkoani Morogoro zilipopamba moto na kuwagusa askari “wale wale” niliowatuhumu kwenye barua yangu, IGP alichukua hatua ya kuwahamishia mikoa mingine!
(iv)           ili kunikatisha tamaa kabisa, barua yangu ya “siri” kwa IGP ikavujishwa kwa makusudi kwenye vyombo vya habari na kuchapishwa kama habari ambayo ilikebehi na kukanusha taarifa nzima niliyotoa, sijui kwa faida ya nani! Lakini huu ni mchezo wa kawaida kwa polisi kwani hivi karibuni Mhe. Waziri Samuel Sitta alipohojiwa na ofisa mwandamizi wa Jeshi la Polisi ofisini kwake, wakiwa wawili tu, taarifa ya kikao hicho ikawa kwenye moja ya magazeti ya mafisadi ikikebehi ushahidi aliotoa Sitta! The integrity of the police force leadership is on the line.
Nimeelezea vizuri katika barua yangu kwa IGP kuwa kundi hilo la mauaji lilikuwa limeelekezwa kuniua kwa kutumia sumu, taarifa ambayo kwa karibu mwaka mzima Polisi hawakutaka kuifuatilia kwa sababu wanazozijua wenyewe.  Sasa huu msukumo mpya wa Jeshi la Polisi kutaka kujua kama nilipewa sumu au la na kukurupuka kutoa tamko hata kabla ya kunichunguza nilivyo, kunihoji mimi na wasaidizi wangu ofisini na hata kuongea na mabingwa wa Kihindi wanaonifanyia uchunguzi, umetokea wapi?  Si ni polisi hawahawa ambao, badala ya kushukuru,  wamekuwa wakikerwa na tahadhari ambazo Waziri Sitta amekuwa akitoa ili suala hili lichunguzwe kwa kina?
Aidha napata taabu kuamini kama DCI Manumba na wenzake waliisoma taarifa halisi ya matatibabu yangu au walisoma taarifa “nyingine”, na kama waliisoma taarifa hiyo wenyewe au “walisomewa”! Nasema hivyo kwa kuwa alichokisema DCI Manumba kwa wandishi wa habari hakifanani kabisa na picha iliyo kwenye taarifa halisi ya Apollo ambayo inatamka wazi kuwa kuna kitu kwenye bone marrow kinachochochea hali niliyonayo, kitu ambacho mabingwa wanahangaikia kukijua, kukidhibiti /kukiondoa huku vyombo vyetu vya dola vikipelekeshwa na mafisadi kusema bila msingi wa kisayansi wala aibu: “hakulishwa sumu”, “hakulishwa sumu”!
Nimesoma darasa moja Kitivo cha Sheria Mlimani na DCI Manumba. Baadaye IGP Mwema alikuwa mwanafunzi wangu wa sheria Mlimani. Vigogo hawa wawili wa usalama wa raia nchini hawajanitendea haki, nao wanajua. Wanajua vilevile kuwa sitakaa kimya au kumung’unya maneno come what may pale ambapo haki inakanyagwa.
Tuendelee kuombeana afya na uhai ili tutendeane haki na vilevile tuitendee nchi yetu haki kwa kuvimalizia viporo vinavyokera vya Dowans, EPA, Kagoda n.k. kwa maslahi mapana ya Taifa letu.
 
Mungu Ibariki Tanzania .

Thursday, February 09, 2012

Mkurugenzi wa TAMWA Ananilea Nkya Akamatwa na Polisi

UPDATE:  Dada Nkya ametoka kwa Dhamana jioni hii!

Dada Nkya akishika bango jana, Picha kwa hisani ya Global Publishers

Kutoka The Guardian:

Senior Tanzanian journalist arrested

The director of the Tanzania Media Women's Association (Tamwa), Ananilea Nkya, was arrested early today in Dar es Salaam.

She was detained along with several activists and journalists during a public demonstration calling for the government to resolve an ongoing doctors' strike.

Several hospitals have been closed during the strike by junior doctors and medical interns, which began on 30 January. They are protesting about pay and working conditions.

Some specialists have also joined the strike, and the Tanzanian government has come under mounting pressure to resolve the dispute.

The reason for Nkya's arrest remains obscure. She did make a statement yesterday about the need "to make the public disabuse themselves of the commonly held belief that prominent people care little about what is going on because they can access medical attention outside Tanzania."

But concerned supporters do not believe that to have been the reason for her detention.
Sources: Daraja/AllAfrica.com/IPPmedia/The Citizen

Monday, October 24, 2011

Polisi Kenya Watoa Onyo Kuhusu Nairobi na Mombasa!

SECURITY UPDATE - PLACES YOU SHOULD AVOID IN NAIROBI

ALERT:

Police have issued a statement giving areas, we should avoid in Nairobi and Mombasa.

In Nairobi

Avoid Corner House, Burger Dome, Ambassadeur Hotel, Akamba Bus, Marble Arch Hotel, River Road, Bus Station and Betty’s Pub.

In Mombasa:

Be on the lookout the Mtongwe ferry and Nakumatt Nyali.

If you must be in these places, be on high alert for suspicious activity or characters.


Report anything un-toward by calling 999 or 112.
The calls go directly to Vigilance House.

Listen to the radio (esp. 98.4 Capital FM Radio Jambo) for more updates as they come.

Stay Safe!

Saturday, April 30, 2011

Uganda Vipi Tena!!!!

Naona waGanda nao wamechachamaa! Habari kutoka Uganda zinasema kuwa watu kadhaa wameuawa jana mjini Kampala. Wengine wameumia jana baada ya polisi kudhibiti umati wa watu waliokusanyika ili kupinga uongozi wa Rais wa Uganda, Yoweri Museveni. Mamia wamekamtwa na polisi. Habari pia zinasema kuwa kiongozi wa upinzani Bwana Besigye ameumizwa vibaya na polisi. Besigye yuko Kenya sasa kwa matibabu.

**************************************************************
(Pichani: FFU wa Uganda wakifanyakazi Kampala jana)

By GODFREY OLUKYA

KAMPALA, Uganda (AP) - Army troops and police fired live bullets at rioting demonstrators Friday, and at least two people were killed and 120 wounded in the largest anti-government protest in sub-Saharan Africa this year.

Rioters burned tires in downtown streets as security forces fired tear gas and guns, and a Red Cross spokeswoman said 15 of the wounded and been hit by live bullets. Battles between protesters and police were also reported elsewhere around the country.

The protests are the first serious demonstrations in sub-Saharan Africa since a wave of anti-government protests swept leaders in Tunisia and Egypt out of power. Ugandan President Yoweri Museveni, who has been in power for a quarter-century, has vowed repeatedly that his government will not be taken down by protests.

The breakout of violence came one day after a brutal takedown of the country's top opposition politician, Kizza Besigye. Police smashed through the window of Besigye's vehicle with the butt of a gun and doused him with tear gas at close range before bundling him into the back of a pickup truck and speeding off.

"They arrested him like a chicken thief. We cannot allow such things to continue. Museveni must go," said Brown Ndese, one of the protesters.

Besigye arrived in Kenya late Friday for medical treatment. He did not speak to journalists at Nairobi Hospital, and an aide said Besigye was physically unable to talk.

During Friday's protests, Red Cross spokeswoman Catherine Ntabadde said at least two people were killed and 120 people wounded. Uganda police spokeswoman Judith Nabakooba said the police were working to contain the demonstrations and did not immediately have a casualty figure.
Some 360 people were arrested, the government said.

Besigye was freed on bail on Thursday but did not make any public appearances or statements on Friday. Radio reports quoted an aide as saying Besigye was in poor health and that he was to fly him out of the country for treatment.

Besigye withstood long volleys of tear gas sprayed directly on him Thursday, but it wasn't clear how sick or injured he was. Attempts to reach Besigye aides for comment failed.

Besigye has held five "walk to work" demonstrations to protest rising prices and what he calls a corrupt government. On Friday, demonstrators carried posters praising Besigye, and questioned why police needed to use violence to arrest him. Opposition members of parliament have demanded an explanation from the government over his treatment.

Ugandan Minister of Internal Affairs Kirunda Kivejinja said at a news conference Friday that police had no intention of arresting Besigye in such a harsh manner on Thursday.

"The way he was arrested was due to the way he reacted," Kivejinja said. "When police advised him not to use a particular road, he instead got out of his vehicle and called his supporters."

About comparisons to Arab uprisings, he said: "Uganda cannot be like Tunisia and Egypt. ... Here we simply have Besigye who does not want to cooperate. He is defiant against lawful orders."
Earlier this month Besigye was shot in the right hand by what he says was a rubber bullet fired by police. He now wears a thick white cast that reaches halfway up his right arm.

Uganda's Daily Monitor newspaper reported on its website Friday that military forces and police fired live ammunition and tear gas at demonstrators in the eastern town of Mbale, some 200 miles (300 kilometers) outside Kampala. Demonstrators fought back with rocks.

The U.S. Embassy in Uganda condemned the escalation of violence and it called on all protesters to obey the law and cease all destruction of property.

"The U.S. Mission in Uganda also urges the Government of Uganda to respect the right of all citizens to peacefully express their views as enshrined by Uganda's constitution. Above all, Ugandan authorities must avoid using excessive force against civilians in this situation. Constructive dialogue is needed now," the U.S. statement said.

Besigye came second in Uganda's February presidential election to Museveni, threatening to end the opposition leader's political career after three straight losses to the longtime leader. Official returns showed Museveni winning 68 percent of the February vote, though Besigye says those returns were falsified and that both he and Museveni got just under 50 percent.

Besigye, though, has had a political resurrection in recent months as the country has seen huge price spikes in food and fuel.

In an interview with The Associated Press at his home last week, Besigye said many Ugandans face a "crisis of survival," that the health care system has broken down and that young people cannot find jobs.

Besigye was the president's personal physician before being dismissed for saying in 1999 the government was becoming a one-man dictatorship.

Uganda is a young country, with half its nearly 35 million citizens under 15. An estimated 1.2 million have HIV/AIDS. The average yearly income is just $1,200, though many here have hopes - and fears - over newly discovered oil that will soon be pumped. An oil curse has befallen other African countries, providing more incentive for corrupt leaders to remain in power in order to steal from public coffers.