Showing posts with label Female Circumcision. Show all posts
Showing posts with label Female Circumcision. Show all posts

Saturday, February 07, 2015

Tamko la Pamoja kwa Siku ya KiMataifa ya Kukomesha Ukeketaji Dhidi ya Watoto wa Kike

10945033_856755441041229_6165141623154796543_o

UNFPA, UNICEF, Shirikisho la Kimataifa la Wakunga na Shirikisho la Kimataifa la Magonjwa ya Wanawake na Uzazi.

Wito kwa wafanyakazi wa afya duniani kote ili kuhamasisha kukomesha ukeketaji

Kwa mwaka 2015, ujumbe wa kimataifa wa siku ya kupinga ukeketaji umewalenga wahudumu wa afya; “Uhamasishaji na ushirikishwaji wa wafanyakazi wa Afya ili kuharakisha kutokomeza ukeketaji”. Na hii ni kwa sababu asilimia 34 ya ukeketaji duniani hufanywa na wahudumu wa afya.

Pamoja na ujumbe huu mahsusi kwa wahudumu wa afya, wadau wengine wote unawahusu.

Ujumbe unasema hivi:

Ukeketaji wa wasichana na wanawake unakiuka haki za binadamu na unadhoofisha afya na ustawi wa wasichana takriban milioni 3 kila mwaka. Zaidi ya wasichana na wanawake milioni 130 katika nchi 29 barani Afrika na Mashariki ya Kati ambapo hadi leo hii vitendo hivi vimekithiri wamekwisha fanyiwa aina fulani ya ukeketaji - na athari kwa maisha yao ni kubwa sana.

Duniani kote, tunashuhudia kuongezeka kwa utayari wa jamii na serikali ili kuondokana na vitendo vya ukeketaji - lakini hii haitoshi kwani jitihada zaidi zinahitajika. Leo, tunapoadhimisha Siku ya Kimataifa ya kukomesha ukeketaji dhidi ya watoto wa kike, tunatoa wito kwa wafanyakazi wote wa afya – kuanzia wakunga, wauguzi madaktari wa magonjwa ya wanawake na watu wote katika sekta ya Afya kutoa hamasa dhidi ya kukomesha vitendo vya ukeketaji wa watoto wa kike.

Mchango wa wafanyakazi wa sekta afya katika jitihada za kimataifa za kukomesha ukeketaji dhidi ya watoto wa kike ni muhimu sana kwani wana uelewa mpana wa mienendo na desturi ya kijamii katika jumuiya wanazozihudumia. Hivyo wafanyakazi wa afya wanaweza kuharakisha kupungua kwa kasi kwa vitendo vya ukeketaji kwani watu wanaowahudumia wana imani kubwa dhidi yao.

Wafanyakazi wa afya pia wana uelewa wa kina juu ya madhara yanayotokana na vitendo vya ukeketaji kwani wanashuhudia madhara katika njia ya mkojo, njia ya hedhi, maambukizi katika via vya uzazi ikiwa ni pamoja na kutoka damu nyingi na hatimae vifo, pia hushuhudia athari za kisaikolojia dhidi ya wale waliofanyiwa vitendo vya ukeketaji hali ambayo ni ya kudumu katika maisha yao.

Wafanyakazi wa afya pia wapo katika nafasi nzuri ya kuongoza jitihada za kupinga mienendo mibaya inayoibuka katika nchi nyingi.

Katika baadhi nchi ukeketaji unafanywa na wahudumu wa afya, mathalan takriban msichana mmoja kati ya watano wamekeketwa na watoa huduma waliopatiwa mafunzo, na katika nchi zingine idadi hii inaongezeka inafikia kati ya wasichana watatu hadi wanne.

Ukeketaji ni kinyume cha sheria katika nchi nyingi, Tanzania ikiwemo chini ya sheria ya masuala ya kujamiiana 1998, na watoa huduma za afya ambao wanafanya vitendo hivyo katika maeneo haya wana vunja sheria. Ifahamike kuwa katika nchi zote, aidha sheria zao ziwe zinaruhusu au haziruhusu vitendo vya ukeketaji ni kukiuka haki za msingi za wanawake na wasichana.

Wataalamu wa afya hususan wale walio katika zahanati na vituo vya afya mara nyingi wanaweza kuwa na shinikizo kubwa la kufanya ukeketaji. Lakini endapo watahamasishwa kupinga shinikizo hilo, wanaweza kuwa sehemu ya ufumbuzi.

Hivyo, kwanza kabisa, tunatoa wito kwa wafanyakazi wote wa afya kama wapo wanaoshiriki vitendo vya ukeketaji kuachana na vitendo hivyo na kutumia ushawishi walionao katika jamii wanazofanyia kazi na kuhamasisha wenzao katika jamii zingine kukomesha vitendo vya ukeketaji katika maeneo yote. Pia tunatoa wito kwa wafanyakazi wote wa afya kulinda afya ya uzazi na ujinsia ya wasichana wote ambao tayari wamekeketwa.

Tunajua kwamba wafanyakazi wa afya hawawezi kufanya hivyo peke yao. Mashirika kama UNFPA, na UNICEF, kupitia mpango wetu wa Pamoja wa kukomesha ukeketaji, pamoja na Shirikisho la kimataifa la Wakunga, na Shirikisho la Kimataifa la magonjwa ya wanawake na uzazi, tuko tayari na tunayo nia ya kusaidia jitihada za kuwapatia wafanyakazi wa afya ujuzi na taarifa yoyote itakayohitajika ili kuongeza kasi katika kukomesha ukeketaji na pia kutoa tiba dhidi ya madhara yaliyotokana na ukeketaji.

Kanuni za kijamii, hususan katika jamii ambazo zina mshikamano na umoja huwa zina nguvu kubwa juu ya maisha na mienendo ya jamii husika. Lakini kanuni hizi zinaweza kubadilika endapo watu wataamua kufanya hivyo. Pia endapo wafanyakazi wa afya, viongozi, wataalam, na, zaidi ya yote, wasichana na familia kwa ujumla, watakemea na kuchukua hatua dhidi ya mienendo mibaya.

Katika Siku ya Kimataifa ya kukomesha ukeketaji, Tushikamane kupinga ukeketaji kwani Afya, Haki na Ustawi wa mamilioni ya wasichana unategemea umoja wetu.

 

Monday, June 30, 2014

Ukeketaji Tanzania - Female Circumcision


FLASH MASSAGE DIASPORA:
 
Kilio cha mwanamziki/mwanahabari mkongwe Freddy Macha hatimaye kimesikika na kuwagusa viongozi wa ngazi zisizokamatika.Ni sawa na kuyaona machozi ya kilio cha njiwa.Kama ni mila,jadi,itikadi za dini kuwepo na utafiti wa kiafya kupunguza maumivu na mateso ya ukeketwaji wa watoto wa kike hata utamaduni wa kambi za jando maporini kwa watoto wa kiume yafanyike kwa madaktari bingwa katika madahawati ya serikali kupitia usimamizi wa kadi za bima maalumu-NSSF kwa jamii kupunguza msongamano
wa vifo kwa watoto ambao kwa miaka ya siku hizi wanazaliwa tayari wamekomaa kama vijana wa Taifa.
   



FREDDY MACHA-KITOTOBLOG
Kumbukumbu:




image

SHEREHE KUSAIDIA UJENZI WA JUMBA LA KUHIF...
Ijumaa tarehe 30 Mei, London. Ukumbi wa hoteli iliyoko kitongoji cha Hackney, kaskazini ya London ulishuhudia usiku wa muziki, chakula na vinywaji. Kila aliyeingi...

Preview by Yahoo


SOURCE: MIKIDADI-DENMARK

Monday, February 10, 2014

Hospitali Maalum Kwa Ajili ya Wanawake Walikeketwa Inafunguliwa!

Hii hospitali itasaidia wanawake waliokatwa Kisimi yaani Tohara!  Kuna kabila mabazo ambazo wanazikata ili ashki ya mwanamke ipungue.  lakini inaleta matatizo wakato wa uzazi.

*************************************
PRESS RELEASE
 
World's 1st Clitoral Repair Hospital for FGM Victims to Open in West Africa on March 7
 
Chantal Compaore, First Lady of Burkina Faso, will preside at the ceremony
 
OUAGADOUGOU, Burkina-Faso, February 10, 2014 -- The world’s first clitoral repair hospital for victims of female genital mutilation (FGM), located in Bobo-Dioulasso, Burkina Faso, will open on March 7, according to a statement released today by the U.S.-based, nonprofit organization Clitoraid (http://www.clitoraid.org). Chantal Compaore, First Lady of Burkina Faso, will preside at the ceremony.
 
 
 
Photo 1: http://www.photos.apo-opa.com/plog-content/images/apo/photos/kamkaso.jpg (The world’s first clitoral repair hospital for victims of female genital mutilation (FGM), located in Bobo-Dioulasso, Burkina Faso, will open on March 7)
 
Photo 2: http://www.photos.apo-opa.com/plog-content/images/apo/photos/nadine-gary.jpg (Clitoraid Communications Director Nadine Gary)
 
Photo 3: http://www.photos.apo-opa.com/plog-content/images/apo/photos/marci-bowers-md.jpg (Dr. Marci Bowers, M.D., and Dr. Harold Henning Jr., M.D., will perform surgeries at the new hospital and also train other surgeons to do it)
 
Photo 4: http://www.photos.apo-opa.com/plog-content/images/apo/photos/harold-henning-md.jpg (Dr. Harold Henning Jr., M.D., and Dr. Marci Bowers, M.D., will perform surgeries at the new hospital and also train other surgeons to do it)
 
The hospital was built with donated funds and through the efforts of worldwide volunteers.
 
“Having Chantal Compaore's support and presence on March 7 is such a wonderful way to celebrate this opening!” said Clitoraid Communications Director Nadine Gary. “She has been a steadfast voice against the horrors of FGM, and we’re honored that she will be there.”
 
Gary said hundreds of women are already on Clitoraid’s waiting list to have the surgery, which will be free for any woman who wants it.
 
“Their wait is almost over,” Gary said. She said the new facility, called “the Kamkaso,” which means “the house for women,” has been nicknamed “the Pleasure Hospital,” since the surgery “will restore their dignity as women as well as their ability to experience physical pleasure, which was taken from them against their will.”
 
Gary went on to explain how the idea of the hospital came about.
 
“After spiritual leader Maitreya Rael heard about a clitoral repair procedure developed by Dr. Pierre Foldes in France, he launched Clitoraid and the idea of building clinics that offer free surgery for FGM victims. After the United Nations adopted a resolution banning FGM, there’s been universal agreement that it’s a violation of human rights and the integrity of individuals. And eliminating FGM  is essential for women’s health, so governments must keep passing laws against it. But Rael realized that it’s also important to repair the damage already caused to living victims. This hospital is the result of his vision.”
 
Gary said Clitoraid volunteer surgeons from the United States, Dr. Marci Bowers, M.D., and Dr. Harold Henning Jr., M.D., will perform surgeries at the new hospital and also train other surgeons to do it.
 
“The goal is to help as many victims as possible have this surgery, which will also help discourage the barbaric practice of FGM,” Gary said.  “When its effects can be surgically reversed for free, what would be the point?”
 
Distributed by APO (African Press Organization) on behalf of Clitoraid.
 

Wednesday, February 13, 2013

Wanapinga ukeketaji wanashabikia Ushoga na Usagaji?


 
JUMATANO wiki hii nilishtuka kusikia mtangazaji wa redio moja jijini Dar es Salaam, akitangaza kuwa siku hiyo ilikuwa siku ya kupinga ukeketaji duniani!

Kilichonishtua ni jinsi ambavyo wazungu kupitia mawakala wao wa kiafrika walivyokomalia hilo tendo la  ukeketaji au tohara kwa wasichana na kulivyolibebea bango, utadhani ni dhambi kubwa kuliko zote duniani.

Wamelikomalia, kila mwaka wanatenga bajeti kubwa kupambana na tamaduni zetu za kiafrika,wakiziita za kishenzi na  sisi tunachekelea kwasababu wanatupa peremende na shanga tunaogopa kuwahoji  vipi ushoga sio ushenzi?

Wazungu wana tamaduni nyingi za kipuuzi ambazo kama ni sisi tungekuwa tunaziendekeza pengine tungeitwa wanyama tusiostahili kuitwa binadamu. 

Wanatenga siku ya kupambana na ukeketaji lakini wao ambao wameathiriwa na vitendo vya ushoga hawataki kutenga siku ya kupinga ushoga na usagaji!

Najiuliza hivi kama vitendo vya ushoga chimbuko lake lingekuwa afrika hawa wakoloni wetu wa zamani wangetudharau vipi,wangetutukana vipi?

Tulidhani kuwa ingekuwa vema wakaja kujifunza kwetu, kufanya utafiti halisi inakuwaje baadhi ya makabila ya kiafrika wanafanya tohara kwa kisu au wembe bila kutumia ganzi na kijana anavumilia halafu anapona bila kutumia dawa ya hospitali?.



Inakuwaje kijana anatahiriwa kwa kisu halafu akitoka damu nyingi anapewa dawa za asili kukomesha damu hiyo na anapona  kabisa bila kwenda hospitalini kutumia madawa ya kizungu?
Hawataki kujiuliza hayo wanaoona tutapewa sifa waafrika wanatulazimisha tufuate kile wanachoamini,kwamba wao hutahiri wanaume wanataka tutahiri na sisi, kwamba wao hawakeketi wasichana na sisi  wanatuzuia. 

Sisi weusi tulizoea tendo la  ndoa hufanywa na jinsia mbili tofauti yaani mke na mme kama mwenyezi alivyoamuru lakini wazungu wamekuja na mapenzi yajinsia moja, yameendelea kushika chati katika miji mbalimbali hapa nchini.

Lakini cha ajaabu ni kwamba wakati utamaduni huo wa kishenzi ukizidi kushamiri katika shule za seminari na kwingineko mitaani, hakuna mkakati wowote wa kupinga vitendo hivyo zaidi ya kusikia wazungu wakitulazimisha tutambue haki za mashoga.

He! yaani hao watenda maovu yanayo mchukiza Mungu na jamii ya wanadamu mnaataka tuwatambue lakini wafrikakudumisha utamaduni wao kwa kufanya tohara mnawambia kuwa utamaduni wao  ni wa kishenzi.

Wafrika  wakioa wake wengi ili  kukidhi haja ya tamaa zao na kuepuka uzinzi wanaambiwa kuwa suala la kuoa wake wengi limepitwa na wakati,lakini kuwa na boyfriend au girl friend ruksa hata kama upo ndani ya ndoa!
 
Suala la kuoa wake wengi limeandikwa hadi kwenye biblia wafalme waliotukuka kama Suleiman walioa wake 700 na hata suala la kurithi ambalo wazungu wanalipiga vita kwa waafrika lilikuwepo tangu zamani.

Sisi tunapojaribu kufanya kile ambacho wazungu hawakipendi tunaambiwa kuwa utamaduni wetu ni wakishenzi wa kwao safi, hata kama wanalala na watoto wao wa kuwazaa.        
Kutokana na upuuzi huo wa kizungu leo katika safu hii nampongeza  kamanda wa Polisi  kanda maalum ya Tarime na Rorya,Justus Kamgisha na wengine waliofanya nzuri kama yeye  kuhakikisha utamaduni wetu unabaki.

Ni kweli na ni wazi kuwa mtu akitenda jambo jema anastahili pongezi akikosea, akosolewe,akiwajibishwa awajibike.
Kamanda wa Polisi wa Tarime/Rorya anastahili pongezi na tuzo ya heshima kwa watu wanaolinda na kutetea utamaduni wetu wa kifrika.
Kamanda huyo  amekataa kupokea mawazo ya kitumwa kutoka kwa mawakala wa kizungu eti azuie wakazi wa wilaya ya tarime kuwatakasa mabinti wao. 
Hiki ni kipindi kigumu ambacho dunia inapitia kuelekea katika utandawazi unaokuzwa na kuenezwa na mabadiliko makubwa ya teknolojia.
Anapotokea mtu kama Kamanda Kamgisha akapuuza amri ya mawakala wa Kizungu waliomtaka kukamata wananchi wa Tarime ambao wangediriki kujihusisha na vitendo vya tohara ya kiafrika, anapaswa kupongezwa.
Kamanda  huyo ameonyesha mfano kwa  makamanda wenzake kuwa unaweza ukatumia akiri kufikiri badala ya miguu au tumbo.
 kiongozi akifanya jema apewe shukrani zake akikosea akosolewe bila aibu, ndivyo leo ninavyoendelea kumpongeza  Kamanda huyo kwa jinsi alivyoshughulikia suala la tohara kwa wasichana wilayani tarime Mwezi Disemba Mwaka 2012.
Hicho ni kipindi ambacho mabinti wengi waliomaliza shule walikuwa wamejiandaa kutahiriwa ili kujiweka tayari kisaikolojia kwa ajili ya kuolewa ,kuposwa kwani tendo hilo huashiria pia ukuaji kimwili.
Kumuingiza kijana wa kiume au kike jando baada ya kumfanyia tohara kunamuepusha na vitendo hatarishi vya ushoga na usagaji, kwani anajitambua yeye ni nani anatakiwa kufanya nini baada ya hapo.
Kijana aliyetahiriwa kwa kisu ni vigumu kumkuta akiwa anajihusisha na utamaduni huo wa kizungu wa kugeuzana, watu wa jinsia moja kufanya yasiyompendeza Mwenyezi Mungu.
Hata hivyo licha ya kwamba utamaduni huo unasaidia kwa kiasi kikubwa kukomesha  vitendo hivyo lakini wenzetu hawapendi wakiona wanatenga fungu la pesa kuwagombanisha raia na serikali yao.   
Wanasema kamateni wote wanaojihusisha na mila hizo kwani zimepitwa na wakati,lakini hawatuambii zilipitwa na wakati kuanzia Mwaka gani.    

Ndipo taarifa zikamfikia Kamanda akitakiwa kuwakamata wale wote ambao wanafanya hivyo,bahati nzuri kamanda huyo ni mtani wa wakurya akitokea Bukoba ikabidi aone aibu akaamua kutumia busara kujumuika na watani zake katika sherehe hizo. 
Kamanda na kupongeza kwa kukataa mawazo  na fikra za kitumwa, umewaruhusu wakazi wa Tarime kuendelea na ustaarabu wao wa kutahiri watoto wa kike.

Hilo ni jambo la heshima kabisa analo stahili kufanyiwa kijana wa kiafrika kwa baadhi ya makabila hapa nchini hivyo,lisingefanyika kama Kamgisha angetumia miguu na tumbo kufikri, kutokana labda na ushawishi wa bahasha.

Nimefurahi nililiposikia kuwa Mkuu wa wilaya ya Tarime Dc.Frank Uhahura alipotoa amri ya kukamatwa wale wote waliokuwa wanakeketa wasichana kama wanavyoita wao, lakini  wewe kwa kushilikiana na vijana wako mkapuuza amri hiyo ili kudumisha amani tarime.
Busara zako, hekima zako zimedumisha amani Tarime kwa gharama ndogo, lakini kama Polisi wangedhubutu kuanza kuwakamata wale wote waliokuwa wanajihusisha na sherehe za jando amani ingetoweka na kuirejesha ingetumika gharama kubwa na umwagikaji wa damu.
Lakini kwa busara zako, Ewe Kamgisha umetambua kazi ya Polisi ni kulinda amani sio kushiriki kuvunja amani, wadau wa maendeleo ya tarime tunaamini kupitia busara hizo unaweza kukomesha mauwaji ya mgodi wa Nyamongo.

Unaweza kukaa na  wamiliki wa mgodi huo mkakubaliana namna ambavyo vijana wa Tarime wanavyoweza kuruhusiwa angalau mara moja kwa wiki kuzoa mawe yanayotupwa kama uchafu ili wao wakasafishe madini ya dhahabu kuliko sasa wanavyoitwa wavamizi.
Mnaweza kukaa mkakubaliana , eneo likaandaliwa ambalo mzungu atakuwa anakwenda kutupa mawe hayo kama dampo ili vijana waende wakaookote kule badala ya kuingia mgodini kama ilivyo sasa ili kuepuka maaafa zaidi.

Nimemalize kwa kuwapa ujumbe waafrika wenzangu hakuna utamaduni wa kishenzi hapa afrika,tunaweza kuungana na wamasai kudumisha utamaduni wetu.