Showing posts with label Abeid Amani Karume. Show all posts
Showing posts with label Abeid Amani Karume. Show all posts

Saturday, January 13, 2018

Mambo Unayotakiwa Kuyafahamu Kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar


Na Jumia Travel Tanzania



Januari 12 ya mwaka huu wa 2018 Wazanzibari pamoja na Watanzania kwa ujumla watakuwa wakiadhimisha miaka 54 tangu kutokea kwa mapinduzi Visiwani Zanzibar mnamo Januari 12, 1964. Mapinduzi ambayo yaliyofanywa na wanamapinduzi wa kiafrika na kupelekea kuung’oa utawala wa kisultani na kiarabu visiwani humo na kuwa na utawala wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

 

Pamoja na siku hii kuadhimishwa kila mwaka, bado kuna watu wengi hawafahamu mambo muhimu kuhusu historia ya Zanzibar na yaliyopelekea mpaka mapinduzi kutokea. Kutokana na umuhimu wa siku hii kwa vizazi vilivyopita, vya sasa na vijavyo, Jumia Travel imekukusanyia mambo muhimu ambayo huna budi kuyafahamu.



Ikiwa na historia ndefu ya utawala wa Kiarabu tangu mwaka 1698, Zanzibar ilikuwa ni sehemu ya nchi ya ng’ambo ya Oman mpaka ilipojitwalia uhuru wake mnamo mwaka 1858 na kuwa chini ya utawala wake wenyewe wa Kisultani.

 

Wakati wa utawala wa Sultani Ali Ibn Said mnamo mwaka 1890, Zanzibar ilikuwa chini ya utawala wa Waingereza mpaka mwaka 1963 ilipowapatia wanzibar uhuru wao, ingawa haikuwahi kuwa chini ya utawala rasmi wa moja kwa moja wa dola ya Kiingereza.



Wananchi wa Zanzibar kwa kiasi kikubwa walikuwa ni mchanganyiko kutoka mataifa mbalimbali kama vile Waarabu, Wahindi, Waajemi, Washirazi na Waafrika, ambapo waarabu na wahindi ndio kwa kiasi kikubwa walikuwa wamehodhi ardhi na shughuli kuu na njia za biashara. Kadri muda ulivyozidi kwenda maingiliano baina ya watu wa mataifa hayo yalizidi kuongezeka kitu kilichopelekea utofauti baina yao kuanza kufifia.


Hata hivyo, walowezi wa Kiarabu kama wamiliki wa sehemu kubwa ya ardhi ya visiwani humo ndio walikuwa ni matajiri kuliko waafrika. Suala hilo pamoja na mambo mengine mengi ni miongoni mwa sababu zilizopelekea waafrika kuona sababu ya kufanya mapinduzi ili kuwa na utawala wa haki na usawa visiwani humo.



Kwa upande wa kisiasa, vyama vikuu visiwani Zanzibar vilikuwa vikiendeshwa na kuungwa mkono kulingana na utaifa (ukabila), kama vile Waarabu walikuwa wakitawala kwa sehemu kubwa ya chama cha Zanzibar Nationalist Party (ZNP) huku Waafrika ilikuwa ni Afro-Shirazi Party (ASP).

 

Baada ya Zanzibar kutwaliwa na utawala wa Kisultani wa Oman mnamo mwaka 1698, sehemu ya ardhi yote visiwani humo iligawiwa kwa wanafamilia wa Kifalme wa Oman, ambapo vizazi vyao viliendelea kuimiliki mpaka mwaka 1964.



Ingawa sio Waarabu wote walikuwa ni matajiri kama familia ambazo zilikuwa zikimiliki mashamba ya karafuu na minazi, hasira ambayo waliyokuwa nayo waafrika ambao walikuwa wakifanya kazi kwenye mashamba hayo ilipelekea kujisikia hali ya kubaguliwa kwenye ardhi yao wenyewe. Hususani kwa kisiwa kidogo kama cha Zanzibar ambapo ilikuwa ni rahisi kuona pengo na utofauti mkubwa kati ya familia tajiri za kiarabu zilizokuwa zinamiliki ardhi na vijakazi wao masikini wa kiafrika.

 

Harakati za kutaka uhuru Visiwani Zanzibar zilianza kutokana na vuguvugu za shughuli za kisiasa ambapo kwa kiasi kikubwa waafrika hawakuwa wanapata uwakilishi sawa na nafasi bungeni. Kuanzia mwaka 1961 na kuendelea kulianza kufanyika kwa chaguzi za kisiasa za kidemokrasia ambapo vyama vikuu vya ASP na ZNP vilikuwa vikichuana vikali.



Chama kilichokuwa kikiungwa mkono na waafrika wengi cha ASP kilikuwa kikiendelea kuungwa mkono na kukubalika miongoni mwa waafrika wengi. Katika maeneo mengi kulipokuwa kunafanyika chaguzi kilionekana kuungwa mkono ingawa matokeo ya uchaguzi yalipotoka yalikuwa yanaonyesha kushinda sehemu chache.



Sababu hiyo ambayo ilikuwa ikijirudia mara kwa mara kwenye kila chaguzi ndiyo iliyopelekea waafrika kuona haja ya kufanya mapinduzi. Mnamo Januari 12, 9164 mapinduzi yalifanyika visiwani Zanzibar na kumfanya kiongozi wa chama cha ASP, Hayati Sheikh Abeid Amani Karume kuwa Rais mpya na kiongozi wa nchi.



Mapinduzi hayo yalipelekea ukomo wa utawala wa kiarabu visiwani Zanzibar wa takribani miaka 200, hivyo kuifanya siku hiyo kusherehekewa kwa maadhimisho maalum na kuwa ni siku ya mapumziko ya kitaifa.  

Saturday, August 30, 2008

Will Smith akutana na Rais wa Zanzibar

Rais wa Zanzibar mh. Amani Abeid Karume akiongea na mcheza sinema wa Marekani Will Smith
Rais wa zanzibar mh. Amani Abeid Karume na mkewe Mama Shadya katika picha ya pamoja na Will Smith na mai waifu wake Jada Pinkett Smith leo huko Ikulu, Zanzibar.
Picha kwa hisani ya kwa mdau Othman Maulidi wa Zanzibar.

Tuesday, August 05, 2008

Muungano - Maoni ya Adamu Lusekelo

Mwalimu Nyerere na Mzee Karume wakikamilisha Muungano 1964

By Adamu Lusekelo
Kutoka: Daily News
Wednesday, July 30, 2008

I first thought that the on-going blah blahing between politicians of the different sides of the political divide in Mainland and Zanzibar would go away. It was too petty to warrant any attention. But, as you know, politicians love attention. They have made it an issue. I haven't.
I find it too silly, to be given such attention. All I know is if some politicians in the islands want out they should be given that opportunity. Let's ask the people of the Zanzibar and Pemba sister islands. Over the years, I have had no problems with unions, especially with my chicks. If they want out, I let them opt out. You can't force someone to love you.
If some politicians in Zanzibar (nchi) want to be called a country otherwise they will commit ‘hara kiri’, then let’s call them 'nchi'. In fact I suggest that we should even call Zanzibar 'nchi' twice. The name should be Nchi Zanzibar Nchi! That way the united republic will be rid of this nonsensical debate.
The United Republic has mega problems. We cannot get water in Dar. I haven't heard anything from the Bunge. Zanzibar has been in the dark for almost two months. I have yet to hear of anyone in the House of Reps fiercely coming down on the Revolutionary Government in Zenj.
Our country is being looted left, right and centre by a cabal of politicians in collusion with international 'investors'. What do you get from the Bunge and the House of Reps? Nothing! Zilch! And now Premier Mizengo 'Pete' Pinda comes with the 'nchi' thing and the whole is awash with this silly debate. It shows how idle some circles in our society are.
I know that politicians have to speak something. But I think they have to speak using their heads, not their mouths! What does the average Zanzibari in Mwanakwerekwe in Zanzibar benefit from being called 'nchi'? Absolutely nothing! What does the average mainlander in Tabora Region benefit from being called Tanzania nchi? If the politicians think they will benefit from making an issue of the 'nchi' thing, they should stand out and be counted. They should stop to manipulate the issue.
Let's just ask the people of Zanzibar and Pemba if they want the Union or they want out – and then let's respect that choice. It is very boring to see politicians, especially in Zenj, wanting to make political kudos out of the Union issue. Be warned people of Zenj, as we are busy wasting people's time talking hot air about 'nchi' thing the people of Pemba are also stirring. They also want out. They want their own government!
And times have changed. You just cannot force a people to love you - not even using guns. For guns have the habit of running out of ammo. Once you run out of ammo the SMG is useless, especially when facing a population armed with 'pangas'. I think it’s about time we revved up the Union and ask the people concerned if they want it or not and not listen to political clowns who want to make political hay out of nothing.
The prices of food are forbidding; and the hospitals are empty with the doctors fleeing abroad. Now they even want to pinch our teachers. Those politicians are making an issue out of being called 'nchi'. That is total nonsense!
UN deputy Secretary General, Asha-Rose Migiro has just told Tanzanians that as far as she was concerned, the UN recognises a country called the United Republic of Tanzania, not Zanzibar! Knowing how silly some of the politicians can be, they must be seething and saying that the UN deputy secretary general should be caned for - saying the truth.
Any way, whatever the outcome of the referendum, I still would like my country, which I love very much, to be called Tanzania. That is whether there is another country called Zanzibar 'nchi' or another country the Republic of Pemba. Just go for it! Predictably, those fellows would go for each other’s throats so fast, they will never know what has hit them.