Tuesday, January 22, 2019
Saturday, January 19, 2019
Kitabu Changu Kutafsiriwa kwa kiSomali

Nimekuwa na mahusiano ya miaka mingi na waSomali wa Minnesota, hasa katika miji ya Faribault na Minneapolis. Nimehusika katika kuwashauri kuhusu maisha ya hapa Marekani, mifano ikiwa ni mihadhara yangu Mankato na Faribault.
WaSomali ambao wamesoma kitabu changu wanakipenda sana na wananikumbusha tunapokutana. Mmoja wao ni rafiki yangu Mohamed Dini. Huyu ndiye tumekubaliana akitafsiri kitabu hicho. Yeye ni mmoja wa waSomali wachache sana wanaotambulika katika fani hiyo hapa Minnesota. Kazi hiyo itaanza mwezi huu.
Ni faraja kubwa kwangu kwamba tafsiri hii itakapochapishwa itapunguza kwa kiasi kikubwa matatizo yanayowakabili waSomali Marekani, ambayo ni mara dufu kuliko yanayowakabili waAfrika wengine wengi. Tofauti na waAfrika wengi, waSomali wengi hawajui kiIngereza ambayo ndio lugha ya Marekani. Vile vile, waSomali ni waIslam, dini ambayo ni ya wachache hapa Marekani, na sehemu nyingi hakuna yale ambayo waIslam wanahitaji kwa mujibu wa dini yao. Kuna juhudi zinafanyika, lakini bado hazijatosheleza.
Ninangojea kwa hamu maendeleo ya shughuli hii hadi ifikie lengo.
Tuesday, January 15, 2019
Saturday, January 12, 2019
Mwongozo wa "Song of Lawino"

Huu ni mwongozo wangu wa pili kuuchapishwa, baada ya Notes on Acebe's Things Fall Apart, mwongozo ambao umekuwa ukitumiwa na wanafunzi na waalimu wa fasihi sehemu mbali mbali duniani kama nilivyowahi kugusia katika blogu hii.
Kila mwongozo unaongelea kazi tajwa lakini pia unagusia kazi zingine za fasihi ili kupanua uwanja wa ufahamu juu ya fasihi. Kila mwongozo unaingiza pia vipengele vya nadharia ya fasihi vinavyohusika katika kazi inayojadiliwa. Kwa hiyo, kwa kusoma mwongozo moja, mtu anajifunza au anapata fursa ya kutafakri mambo mengi.
Nina nia ya kuandika miongozo mingine ya kazi muhimu za fasihi ya Afrika. Unaweza kujipatia mwongozo huu mpya na vitabu vyangu vingine katika duka la mtandaoni
Friday, January 11, 2019
Wanachuo wa Gustavus Adolphus Wameenda Tanzania

Nimekuwa nikialikwa kila mara kuongea nao kuhusu masuala ya tofauti za tamaduni kutokana na kwamba wanasoma kitabu changu, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences, na tunapokutana wananiuliza maswali yatokanayo na niliyoandika au mengine. Maswali yalikuwa ya aina mbali mbali, yakiwemo kuhusu mtazamo wa waTanzania juu ya waMarekani na pia kuhusu hali ya kisiasa Tanzania.

Subscribe to:
Posts (Atom)
Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault
Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...

-
Leo ni kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa kwangu, ambayo ni tarehe 17 Agosti, 1951. Familia yangu, ndugu, na marafiki wamejumuika nami kushereh...
-
Leo napenda kukitambulisha kwako mdau kitabu muhimu cha ki-Swahili, Tenzi Tatu za Kale . Nilinunua nakala yangu miaka kadhaa iliyopita katik...
-
Kutafsiri kazi ya fasihi ni kazi ngumu ya kuchemsha bongo. Inahitaji ufahamu wa hali ya juu wa lugha husika, na pia hisia makini za kifasih...